Ni rasmi sasa ombi la wafanyabiashara wote wa Kariakoo kushiriki mkutano na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa limekubaliwa ambapo sasa utafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wafanyabiashara hao ambao awali walipaswa kutoa wawakilishi wao kwenye kikao na Waziri Mkuu walikataa pendekezo hilo huku wakishinikiza uwepo wao wote ili kuleta tija ya maamuzi ya mkutano huo.
Mmoja wa viongozi wa wafanyabiashara hao (jina lake halikupatikana kwa haraka) ambaye alifanya kikao cha ndani na baadhi ya viongozi wa Serikali alitoka nje na kutoa tamko kuwa wafanyabiashara wote watashiriki mkutano na Waziri Mkuu.
