Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania *Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan* leo September 18 ameweka Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya kiwango Cha lami yenye Urefu wa Km 53.2 kutoka Ruangwa-Nanganga ambapo amemtaka Mkandarasi wa ujenzi huo kukumilisha ujenzi kwa Wakati.



Akizungumza na Wananchi wa Kijiji Cha Nandagala ilipofanyika Shughuli hiyo *Rais Dkt, Samia* amesema lengo la Serikali ni kuunganisha Mkoa wa Lindi kwa Barabara za lami na Barabara za kuunganisha Wilaya.



Pamoja na hayo *Rais Dkt, Samia* amewahimiza Wananchi wa Lindi kuweka mkazo kwenye kilimo Ili kuinua uchumi wa Taifa na mkulima mmojammoja.