Mkurugenzi wa Taasisi ya

Nasimama na

Binti Wema Sepetu ameahidi

kutoa

madawati 50 kwenye Shule tatu alizotembelea

Wilayani Pangani Mkoani Tanga ambapo amegawa pia zawadi mbalimbali katika

Shule hizo zikiwemo jezi, daftari pamoja na kalamu ili

kuwasaidia Wanafunzi hao kusoma kwa bidii na

kusaidia uboreshaji wa elimu.





Wema ametoa ahadi hiyo baada ya yeye pamoja

na Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah pamoia na  watu wengine

akiwemo Msanii Maarifa walipotembelea na kuongea

na Wanafunzi wa Shule za Sekondari Kipumbwi na

Mwera, Bushiri, Kimanga zilizopo Wilayani Pangani.

Kwa upande wake DC Zainab amesema

wametembelea Shule hizo katika mendelezo wa

kampeni ya Niache nisome Pangani inanitegemea

ambayo inalenga kuhamasisha

ukuaji wa elimu Pangani, kampeni hiyo itahitimishwa

kesho na itahudhuriwa na Viongozi mbalimbali.



Akiongea na Wanafunzi hao DC Zainab amesema


"Mnapaswa kuongeza bidii kwenye elimu ili

mufanikiwe zaidi na kutimiza ndoto zenu, tuna

Viongozi wengi Vijana kwenye Nchi yetu, walisoma

na ndio maana wamefika hapa, niwaombe muweke

msukumo mkubwa kwenye masomo yenu ili tuwe na

Taifa lenye wasomi wengi"