JamiƬ imehamasishwa kushiriki katika Tamasha la

Maendeleo la kutangaza Fursa za Kiuchumi na

Kupinga Ukatili (ZIFIUKUKI) lenye lengo la kuileta

Jamii sehemu moia kupata elimu na huduma

mbalimbali za kiiamii.


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na

Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ametoa

rai hiyo wakati akizungumza na waandishi wa Habari

jijini Dar Es Salaam ambapo

amesema Tamasha hilo litafanyika kwenye Mikoa

mbalimbali nchini (imetajwa).

Dkt. Gwajima amesema jukumu la kuzuia vitendo vya

ukatili ni la kila mwanajamii na kila taasisi hivyo

Wizara inashirikiana na Wadau mbalimbali kuelimisha

jamii kupinga ukatili na kufikia fursa za kiuchumi ili

kutokomeza umaskini ambapo pia huchochea ukatili.


Aidha ameiomba Ofisi ya Rais- TAMISEMI kupitia

viongozi wa mikoa husika kulipokea Tamasha hili na

kuwaelekeza Maafisa Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii kushiriki kuratibu Matamasha hayo katika

Mikoa na Halmashauri.