Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mhandisi  Felchesmi Mramba amesisitiza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuendelea kufanya tafiti zaidi ikiwemo kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu uwepo wa madini mbalimbali nchini



Mhandisi Mramba amebainisha hayo leo Julai 3, 2023 alipotembea  banda la Wizara ya Madini, Taasisi za Wizara na Wadau wa Sekta ya Madini  katika Maonesho  ya Kimataifa ya Sabasaba jijini Dar es Salaam.



Aidha, ameishauri GST kusambaza vitabu vya Madini  yapatikanayo  Tanzania toleo Jipya 2023 kwa wananchi  ili waweze kutumia taarifa hizo ambazo ni muhimu.



Mbali na GST ametembelea washiriki mbalimbali katika Banda la Wizara.