Warembo 20 kutoka Kanda na Mikoa mbalimbali wa Shindano la Miss Tanzania watarajiwa kuingia kambini  ambapo maudhui ya Shindano hilo linatarajiwa kuruka Mubashara Julai 26,2023 st bongo kwenye King'amuzi cha Startimes. 



Akizungumza na Wanahabari Leo Mei 31,2023  Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema kwa mara ya pili mfululizo wanaendelea kuunga mkono Shindano hilo la urembo ambapo linawapa nafasi wasichana kutimiza ndoto zao kupitia tasnia ya urembo. 



"Jukwaa la urembo limekuwa likifungua fursa mbalimbali kwa warembo hivyo kampuni ya Startimes itaendelea kutoa mchango kwa warembo hao ambapo mara nyinyi wamekuwa wakisaidia jamii zao kupitia talanta zao."