Akizungumza na Wanahabari Leo Mei 31,2023 Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema kwa mara ya pili mfululizo wanaendelea kuunga mkono Shindano hilo la urembo ambapo linawapa nafasi wasichana kutimiza ndoto zao kupitia tasnia ya urembo.
"Jukwaa la urembo limekuwa likifungua fursa mbalimbali kwa warembo hivyo kampuni ya Startimes itaendelea kutoa mchango kwa warembo hao ambapo mara nyinyi wamekuwa wakisaidia jamii zao kupitia talanta zao."


